PLANET BONGO KILA JUMAMOSI SAA NNE ASUBUHI EAST AFRIKA RADIO NA KILA JUMA TANO SAA TATU KAMILI USIKU EATV.
KUWA MAKINI
TULIA NA MMOJA UNAYE MPENDA, ACHA NGONO ZEMBE
POWER JAMS
POWER JAMS,JUMATATU MPAKA IJUMAA KUANZIA SAA 7 MCHANA HADI 10 ALASIRI EAST AFRICA RADIO.
MATING'A
DEEJAY AD a.k.a MAFUVU.
KUTANA NA DEEJAY AD KWENYE POWER JAM KILA J.3 NA ALHAMISI (1:00 - 4:00 pm), THE CRUISE J5 (8:00-9:00 pm), PLANET BONGO JUMAMOSI (10:00 - 12:00 pm) & FNL. NDANI YA EAST AFRICA RADIO & TV, TING'A KALI NAMBA MOJA KWA VIJANA
Baada ya mchiz kukamua bongo pale makao makuu ya Zain ikafikia time ya kwenda Mwanza, Arusha kisha kurudi tena Bongo...
Dj Mafuvu, Domonicky Nyalifa na Dullah... hapo ni Airport tayari kabisa kukwea pipa mpaka Mwanza kwa ajili ya show ya J Martins.
Kelvin Twiser na J Martins story kidogo kabla ya kusepa kuelekea Mwanza.
Dj Kim akiwa kwenye mstari kabla ya kukaguliwa na kukwea.
Dullah na J Martins..
Dickson na Ngali.. hivi ni vichwa vingine kutoka EATV ingawa huwa hauvioni kwenye kideo.
Hawa ni jamaa wa Zain ambao nao pia walikuwa kwenye huo msafara wa kuelekea Mwanza
Dullah ndiye alikuwa mc wa show zote Mwanza, Arusha na Dar.
Time ya kuondoka ikafika tukawa tayari kuelekea kwenye ndege kwa ajili ya kuitafuta mwanza, ilikuwa safari ya kama saa moja na dakika hamsini na tano hivi.
Leo kitanukishwa Mwanza ndani ya Villa Park, kesho itakuwa Arusha viwanja vya Triple A na kesho kutwa yaani juma pili itakuwa Dar-es-salaam bata zitaliwa pale Billicanas.. UHURU UNAO SASA.
Mmoja wa member anayeunda kundi la Wakali Kwanza, Joseph Mapunda a.k.a Qj pichani akiwa na mkewe Bi Elizabeth na kwa sasa wameungana na kuwa kitu kimoja kama Mr and Mrs Joseph Mapundahii ni juzi tu jamaa kavuta jiko safi.
Huyu ni Matonya siku ya harusi yake hapo akiwa na rafiki yake kipenzi Banana Zoro pamoja na mkewe.. Na kwa kudra zake mwenyezi mungu ndoa hiyo imeshaipa baraka kwa kupatikana mtoto.. Tonya pia ni moja kati ya wasanii wa bongo flava ambao tayari washauwaga ukapera.
Picha juu ni Juma Nature na mkewe Pili siku ya harusi yao .. Sir Juma Nature na mkewe wamebarikiwa kupata mtoto wa kike aliyezaliwa katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke.. Huyu ni Mwingine pia ambaye amesha watoroka wale wengi ambao bado hawajakamilisha hili.
Baada ya vikao vingi vya kukamilisha hili na kupanga jinsi ya kulikamilisha hatimaye siku ikafika na kijana kutoka TMK Wanaume Family kuuwaga rasmi ukapera na kutuletea shemejiiiii.....!!! Ilikuwa siku ya jumamosi baada ya kuchukuwa kifaa jumla, hii ilikuwa katika kanisa la Azania Front jijini Dar es salaam.
Judith Wambura alizaliwa mkoani Shinyanga tarehe 15 jun, 1979 kwa Martha na Lameck Isambua Mbibo ambao ndio wazazi wake. Inasemekana dada jide alianza kuimba akiwa na umri wa miaka saba, alianza kuimba kanisani kama ilivyo kwa wasanii wengi, bi shosti pia ni moja ya wasanii wa bongo flava wanaoishi kwenye ndoa kwa sasa.
Banana Zorro na Suzy Walele wakilishana keki siku ya harusi yao iliyofanyika katika ukumbi wa Msasani Beach Club jijini Dar - es- salaam. Banana pia ni masanii wa bongo flava ambaye amesha sepa kwenye kundi la ukapera.
Na kwa sasa nadhani huyu ndio atakaye fata tunamuombea kila la kheri mungu ampe wepesi katika hilo Amin inshaallah.
NI WEWE KAMPENI, MAENEO YA ITUNUNDU PAWAGA JANA
-
Ni Wewe ni kampeni iliyozinduliwa na redio Ebony FM iliyoko Nyanda za juu
kusini, ikiwalenga zaidi wananchi wa vijijini ambao miundo mbinu ya umeme ...
HARD PRICE COMING SOON
-
* Samahanini sana wadau wangu... Naombeni sana mnisamehe kwa kupotea kwa
kipindi kirefu, na yote haya yanatokana na majukumu ya hapa na pale. Ila
nisinge...