.

Tuesday, September 7, 2010

SIKILIZA.....SUNDAY SOUL @ EAR KILA JUMAPILI!


SIKILIZA EAST AFRICA RADIO KILA JUMAPILI SAA 10 - 12 JIONI KWA NGOMA KALI ZA LONG TIME KAMA SHOULD I SAY YES,NIGHT SHIFT,LET'S GO DANCING,ELLUSION NK NA DJ 45 KING...WAY BACK HITS!

Monday, September 6, 2010

MPANGO MZIMA.....IIISSSSTAAAAFFFIIIKAAAA TTTTTTVVVV!


Lile ting'a kali no 1 si ndo' limerudi tena babu....kila siku za Jumatatu na Alhamisi mida ya saa 3 usiku usikose kukodolea mimacho runinga yako Live!!!!


WAKALI CHRIS BROWN NA T.I NDANI YA MOVIE MPYA

Wana toka kwa Obama,Chris Brown na T.I wamepata shavu kwenye movie mpya ya TAKERS ambayo imedondoka kitaani tangu Agosti 27 2010

......Sasa Mpango Mzima si ndo' huo sasa au hii tuite Mtoni Movie kwetu si tunaita Bongo Movie au!!!

TIP TOP KUDONDOSHA ALBUM MPYA IDD!

Rais wa Manzese,Madee ataliongoza baraza lake la wasanii siku ya Idd pande za Club San-Siro maeneo ya Sinza kwenye uzinduzi wa album mpya ya kundi BADO TUNAPANDA.

Wana watasindikizwa na vichwa vikali kama Godzilla,Jahfaray,Mwasiti,Lina,Young D na Roma.

Sunday, August 22, 2010

KIDEO CHA LINEX KINAGONGWA LEO..!!

Ni jamaa ambaye amelalamika sana kuhusu mama watoto wake anafahamika kwa jina la Mama Halima kuwa amemtenda sana na hakutegemea hilo kwa bi shosti huyo.

Mchiz anaitwa Linex ambaye ngoma yake ya Mama Halima inafanya vzr sana kwa sasa kwenye Radio station nyingi za hapa bongo.

Sasa mpango mzima ni kuwa kideo cha ngoma hiyo kinachapwa leo na mtu mzima JOHN KALLAGE na siku si nyingi kitaanza kuwa hewani kupitia EATV..

Thursday, August 12, 2010

SSSHHHH... KIJANA ACHA KULALAMIKA TUMIA KURA YAKO..!!


Telavisheni ya Afrika Mashariki (EATV) na East Afrika Radio kwa pamoja zimezinduwa kampeni ya kuhamasisha vijana kushiriki kikamilifua katika zoezi la upigaji kura katika uchaguzi mkuu wa oktoba mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana jijini Dar es salaam, kampeni hiyo ilizinduliwa katika kipindi cha 5 connect kilicho rushwa moja kwa moja kuanzia saa moja usiku na kuhudhuriwa na wageni vijana pamoja na mjumbe kutoka Tume ya Uchaguzi.

Kituo cha EATV ambacho ndio kituo namba moja kwa vijana na kimechukuwa jukumu hilo kuwahamasisha vijana kutumia kura yao, kutokana na utafiti uliofanywa na kituo hicho kuonyesha kuwa vijana wengi hawashiriki katika kupiga kura.

Katika kufanikisha hilo vituo vya EATV & EAR vitakuwa vinatumia ujumbe wa 'KIJANA ACHA KULALA MIKA TUMIA KURA YAKO' na ujumbe huo utakuwa ukirushwa hewani kupitia televisheni ya EATV na East Afrika Radio.

Ujumbe huu unalengo la kuhakikisha kijana anachaguwa kiongozi bora badala ya kuwaachia wengine shughuli ya kuchaguwa viongozi na badala yake kuishia kulalamika pindi wanapoona uamuzi mbali mbali wa viongozi unawaathiri.

Kampeni hii ambayo tumetumia picha za video na sauti za vijana mbalimbali itaendelea hadi Oktoba 30 na vile vile ifikapo septemba tutazinduwa kipindi maalum kwa ajili ya uchaguzi kiitwacho UCHAGUZI XPRESS LIVE.

Kipindi hicho tutajadili mada mbalimbali zenye lengo la kumjenga kijana ufahamu kuhusiana na umuhimu wa yeye kushiriki katika uchaguzi mkuu ili waweze kuchaguwa viongozi bora na wenye sifa.

Friday, August 6, 2010

WANA WEEKEND NJEMA...ILA GAMBE KIAINA AU VP!!!!

MWANA KUGOMBEA U-PREZIDAA!

Wyclef Jean mwana toka Haiti ametangaza nia ya kugombea urais wa Haiti utakaofanyika mwezi November tarehe 28 mwaka huu...Kila la heri!

Tuesday, August 3, 2010

WATENGWA WAMKUMBUKA FAZA NELLY!

RIP NELSON CHRIZOSTOM BUCHARD AKA FAZA NELLY (1976-2006)

Kundi la Watengwa toka A-Town chini ya JCB wametoa audio na video ya kumkumbuka mwanaharakati na memba wa X-Plastaz,Faza Nelly ambaye alifariki 29 March 2006 kwa kuchomwa kisu Mkoani Arusha iitwayo "SITOWASAHAU MILELE"

Ndani ya ngoma hiyo pia wamekumbukwa wanaharakati kibao wa muziki wa Tanzania (REST IN PEACE..BROS & SISTAZ)

Tuesday, July 27, 2010

Saturday, July 24, 2010

MWANA ADAI KAIBIWA BEAT YA "USIJE MJINI"

Mchizi anajulikana kama Nazir Ally AKA Naz D (shati jekundu) toka pande za Zenji ameibuka na kudai kuwa Beat ya Usije Mjini ambayo wana AY & FA wametia mavocco humo ndani ni mali yake na aliinyonga Producer Pancho na Pancho ameitoa bila ridhaa yake,na yeye kudai kua haina kwere ila yeye nae atatoa ngoma kwa beat hiyo hiyo.....na atakuja mjini na track yake!!!

Wednesday, July 14, 2010

AL BATA...MARUFUKU KULIWA ZENJI!

Wimbo wa Mhhhh Mhhhh....Al Baaaataaaa toka kwa Offside Trick umepigwa marufuku visiwani Zanzibar.

Kwa mujibu wa mmoja wa memba wa kundi hilo,Lil Ghetto wimbo wa Al Bata umepigwa marufuku kupigwa kwenye Radio Stations zote,Night Club,pamoja na Video yake pia kutokuoneshwa na tangazo hilo pia limetolewa kwenye runinga ya TVZ.....Nyunyuz zinadai kuwa hata wimbo wa "AHMADA" nao umefungiwa kwa kua eti unamlenga mmoja wa kiongozi wa ngazi za juu visiwani humo....NISIJE NIKAKOSA MIEEEEE.....NIKAKOSAAAAA!

TEENS...YOUTH....DONT MISS THIS..!!!

We need new leaders of industries and God is putting you up in that position...don't Miss out this!......Teens.....Youth.....are gonna be in the House.....come and hear Words that will change your Destiny... ....new politician are been raised and you are among them ,new Doctors ,Business men and women....The future is yours....Your a Doctor with a difference...a lawyer with a difference...a manager with a difference.....an accountant with a difference a banker with a difference...I know who i am........The future is mine......Glory to God...!!!!!!!

don't Miss this Special online Conference with Pastor Chris..Teens and Youth around the World will be connected on that Day be a apart of this great movement.

Bring a long with you, Your brothers and sisters..your cousins, your Children...your friends Children, your big sisters and big brothers, your friends...your friends friends...Ur Future will never remain the same

Come and experience The Word The praise and Worship,The Dancing and Drama...Free Drinks and Snacks will be available also ..............

BREAKING NEWS...ABUU FLAVA NINI TENA!!


Msanii Chipukizi wa Bongo Flava,Abuu Flava ameshitakiwa COSOTA na Mwanamuziki Diamond kwa kosa la kutoa wimbo wake wa Kafara ukiwa unafanana melody na ule wa Diamond,Mbagara.

Na jana ndio ilikua ni siku ya kutolewa hukumu japo Diamond hakufika hata siku moja kwenye kikao cha usuluhishi...na haya yalifikiwa...

1. COSOTA watatoa matangazo kwa FM Radio zote kupiga marufuku wimbo wa KAFARA usichezwe tena!

2.Itabidi Abuu Flavaa amlipe fidia msanii Diamond kama akitaka.

POLE MWANA BUT KAMA KUNA PRODUCER YOYOTE YUKO TAYARI KUMSAIDIA DOGO KIMUZIKI AWASILIANE NAE KWA No: 0652131651 KWANI ANA TALENT NA ANAWEZA KUFANYA VIZURI KWENYE GAME!!!!!!!!

Tuesday, July 13, 2010

MMHH...MWENZANGU!

....Hata Tabolaaa hamna hiii!!!!

DUH...MWANA ALITAKA KUSEPA NA WORLD CUP??




PWEZA ATUNUKIWA KOMBE LA DUNIA

Pweza aliyejipatia umaarufu duniani kwa kutabiri "mia" mechi za kombe la dunia 2010,Paul ametunukiwa kombe la dunia na mmiliki wake anasema kwa sasa amestaafu utabiri na anakula bata tu....kwenda mbeeeeleeee!

CHAMELEONE NA SHAKIRA DAM DAM!

Mwana toka Uganda,Jose Chameleone akiwa na Shakira kwenye maandalizi ya show ya fainali la kombe la Dunia 2010 na alipiga show ya kutakata...hakwenda na maji!

NAMELESS AZUSHIWA KIFO!

Habari zilisambaa jana kwenye mtandao wa Facebook kuwa Nameless amepata ajali mbaya ya gari Mombasa lakini habari za kuaminika zinasema mwana mzima wa afya na yuko Malindi akijiandaa kupiga show kadhaa...POLE JO!!!

Monday, July 12, 2010

WAHU NAE ALA BATA KWA OBAMA



Shemeji yetu kwa Nameless,Mwanamuziki Wahu toka Kenya yuko kwenye tour nchini Marekani.
Si unakumbuka mipini ya Sweet Love na Running Low?...hapo juu wana wakilishwa bata mjini Kansas na atakua huko kwa wiki tatu..!

BATA ZA AY & FA...NDANI YA ULAYA!!!

SPAIN BINGWA WA DUNIA 2010

Nahodha wa Spain,Iker Casillas akinyanyua Kombe la Dunia baada ya kuibonda Timu ya Holland 1 - 0

Thursday, July 8, 2010

CHAMELEONE NA BEENIE MAN WATOA NGOMA!

Jose Chameleone toka Uganda na King Of DanceHall,Beenie Man "mjukuu wa Baba T" toka Jamaica wametoa ngoma kali iitwayo..."How We Go" wakiwa wamempa shavu Jacky toka Blu 3.

Chameleone na Jacky walitupia ma-vocco Dreams Studio-nchini Uganda na kuyapeleka Jamaica na Beenie Man kumalizia mpango mzina na mzigo kwa sasa inapata shavu la kutosha kwenye redio nchini Uganda......................na kupitia EA Radio utaisikia kwa mara ya first!!!

..WE USIJE MJINI...WAO WANAENDA ULAYA!!!

...Hivi ni kweli wewe USIJE MJINI halafu wao wanakwenda kupiga Tour Europe???!!

"Mapacha Wasiofanana" Mwana Fa na AY wanatarajiwa kuondoka next week ya wiki ijayo kwenda Ulaya kwenye nchi za Finland,Holland,Denmark,Norway,Italy
na Sweden kuwahamasisha watu wasije mjini ambapo watakua huko kwa zaidi ya mwezi mmoja wakipiga show ya Hip hop ya kutakata...

Kila la kheri wana,Mpeni hi 'PWEZA WA UJERUMANI' mkikutana nae,nasikia yu waishi huko!!!



Wednesday, July 7, 2010

DUH...REGGAE INAPOKUTANA NA BOLINGO!!!

Mkali toka Kenya,Wyre amepiga collabo na Mwanamuziki Mkali wa KwasaKwasa toka Congo DRC,Kanda Bongo Man.
Wyre na Bongoman walikutana nchini Sudan kwenye tamasha la Miss Malaika na Bongo Man kuzimia show ya Wyre na kumuomba wapige collabo...Wyre ameshapeleka "Vocal" zake nchini London kwa Producer wa Kanda Bongo Man na tunasubiri mating'a yawe tayari ili mpango mzima uwekwe hadharani...Duh reggae inapokutana na bolingo!!!

Thursday, July 1, 2010

SUGU KUGOMBEA UBUNGE!

Kalapina-Udiwani,Kinondoni-CUF

Nakaaya-Ubunge,Arusha-CHADEMA

Sugu-Ubunge,Mbeya Mjini-CHADEMA

Mkongwe wa Hip Hop Tanzania,Joseph Mbilinyi AKA Sugu ambaye amejinga na CHADEMA hivi karibuni,ametangaza nia yake ya kugombea Ubunge kwa tiketi ya CHADEMA,jimbo la Mbeya mjini.


Kwa sasa Mheshimiwa mtarajiwa yuko Mkoani Mbeya akiwa kwenye mchakato wa kurudisha fomu baada ya kupata ridhaa ya chama chake...Sugu anaungana na wasanii wengine toka Tanzania kama Kalama Masoud AKA Kalapina anatakayegombea Udiwani jimbo la Kinondoni-DSM kupitia chama cha CUF,na Nakaaya Sumary aliyetangaza nia ya kugombea Ubunge mkoani Arusha kwa tiketi ya CHADEMA...Hatutauza kura zetu....ila Kila la Kheri waheshimiwa watarajiwa!

Wednesday, June 30, 2010

HEAVY WEIGHT MC....KUPIGA SHOW KWA OBAMA!

Joseph Haule AKA Mwana wa msolopa gazi AKA Mti Mkavu AKA Mc shupavu AKA Heavy Weight MC AKA Mr red carpet AKA Mwanaharakati..(Mhh hiyo yangu) ...Mwezi huu anaanza Hip Hop Tour yake ya kimuziki nchini Marekani.

Na hii itakua ni tour yake ya kwanza kupiga kwa Obama tangu aanze game rasmi zaidi ya miaka 15 iliyopita,na ataanza kuwasha moto tarehe 4 July,Houston-Texas..wana wa kwa Obama watasikia live track kali za Hip Hop kuanzia Chemsha Bongo,Bongo-Dsm,Nikusaidiaje,Zali la mentali,Sauti ya Ghetto,Msilie na hits kibao....Hapo Vipi???..Hapo Sawaaaaaaaaaaaaaaaaaaa...............!

MAMA NA MWANA !

Nazizi Hirji AKA Mama Tafari akiwa na mtoto wake wa kiume,Tafari baada ya kujifungua hivi karibuni....kushoto ni kama shemeji yetu ambaye jina kapuni,au nitamuuliza JahFaray kama kweli ndio huyu shemeji yetu!

SWALI LA KIZUSHI...Je mtoto Tafari nae atakua na DreadLocks kama Nazizi????!...Hongera JahFaray (mzee wa wali nazi) kwa kupata mjomba!!!

Monday, June 28, 2010

BATA ZA MB DOG SASA ZATAFUNIWA UNYAMWEZINI

mb dogg amesafiri kuelekea uingereza kwa ajili ya show ambazo zitachukua takriban wiki tatu. akiwa huko atapafom ktk mij tofaut ukiwepo milton keynes, bss onx bristol, pia birmingham.

pia hakuwaacha bure wabongo amewaachia track yake ambayo iko ktk albam yake ya pili ya akili yangu track inaitwa kilio changu. kwasasa mbdog yuko ktka hatua za kumalizia albam yake ya tatu na soon atatambulisha singo yake mpya ambayo amemaliza kurekodi usiku wa kuamkia tar 25. mbdogg anaashukuru mashabik wake wote wanaomsapot ktk game.

Thursday, June 24, 2010

REST IN PEACE MICHAEL JACKSON!!!

Leo 25 June 2010 imetimia mwaka 1 tangu mfalme wa Pop dunuani,Michael Joseph Jackson aiage dunia akiwa na miaka 50.

Mwana alianguka ghafla akiwa mazoezini akijiandaa na show yake ya "THIS IS IT" iliyokua ifanyike nchini Uingereza na madaktari walisema kutumia kwake madawa ya kutuliza maumivu ndiyo yaliyosababisha kifo chake na kupelekea daktari wake Conrad Murray kuingia matatani.

REST IN PEACE (KING OF POP) MICHAEL JACKSON!

HIVI MLISEMA HASHEEM THABEET MREFU EEENHHH?!!


Hasheem Thabeet,Memphis Grizzliers (urefu Futi 7.3)

Manute Bol akila tizi

Marehemu Manute Bol (urefu Futi 7.7)

Mwana anakwenda kwa jina la Manute Bol,raia wa Sudan aliyekua anacheza basketball ligi ya NBA-Marekani na amemzidi Hasheem Thabeet kwa inchi 4.

Alichezea timu za Washington Bullets,Golden State Warriors,Philadelphia Sixers na Miami Heat kuanzia 1985 na alistaafu 1994 na akafariki dunia June 19,2010

....REST IN PEACE...TOLU!

Monday, June 21, 2010

KAMA UNA MKWANJA...SEMA NA BONTA!

Mwana toka pande za A-Town na kundi la RiverCamp Soldiers,Bonta alipiga show pande za TCC Chang'ombe na kuimba na wana mwanzo-mwisho track yake ya Nauza Kura Yangu...Na kama una mkwanja anauza kura yake si unajia uchaguzi October????!!!

Saturday, June 19, 2010

KAMA VP...WEEKEND NJEMA!!

Halafu kama ni Bataaaa,basi kiainaaaaaaa au vpppp.........MIIIAAAAAA!!!!

NAZIZI AKA MAMA NANILIII!!!!

Nazizi

Mwanadada Nazizi toka Kenya anayeunda kund ila Necessary Noise na Wyre,Pamoja na lile la East Africa Bashment Crewinasemekana amejifungua hivi karibuni baada ya kuolewa kwa siri kwa zaidi ya miaka 2 sasa huku siri hiyo ya kuolewa kwake ilikua inajulikana kwa watu wake wa karibu wa familia tu...!

KILA KHERI SISTEE....MIAAAAAA!

Friday, June 11, 2010

...KAMA VP...TUKUTANE LEO UCKU,KEMPINSKI-LEVEL 8!!!


Lile bata la kufa mtu limerudi tena ndani ya Kempinski,Level 8.
Mpango mzima utamhusu Dj mkali toka Kenya,DJ Pinye na Crew nzima ya EA Radio DJs kuanzia saa 3 ucku itakua After Party ya ufunguzi wa World Cup 2010....!

...BROTHERZ & FLOWERS.....CU THERE....!