.

Thursday, April 15, 2010

HAWA NDIO BAADHI YA WASANII WALIO UWAGA UKAPERA.

Mmoja wa member anayeunda kundi la Wakali Kwanza, Joseph Mapunda a.k.a Qj pichani akiwa na mkewe Bi Elizabeth na kwa sasa wameungana na kuwa kitu kimoja kama Mr and Mrs Joseph Mapunda hii ni juzi tu jamaa kavuta jiko safi.

Huyu ni Matonya siku ya harusi yake hapo akiwa na rafiki yake kipenzi Banana Zoro pamoja na mkewe.. Na kwa kudra zake mwenyezi mungu ndoa hiyo imeshaipa baraka kwa kupatikana mtoto.. Tonya pia ni moja kati ya wasanii wa bongo flava ambao tayari washauwaga ukapera.


Picha juu ni Juma Nature na mkewe Pili siku ya harusi yao .. Sir Juma Nature na mkewe wamebarikiwa kupata mtoto wa kike aliyezaliwa katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke.. Huyu ni Mwingine pia ambaye amesha watoroka wale wengi ambao bado hawajakamilisha hili.


Baada ya vikao vingi vya kukamilisha hili na kupanga jinsi ya kulikamilisha hatimaye siku ikafika na kijana kutoka TMK Wanaume Family kuuwaga rasmi ukapera na kutuletea shemejiiiii.....!!! Ilikuwa siku ya jumamosi baada ya kuchukuwa kifaa jumla, hii ilikuwa katika kanisa la Azania Front jijini Dar es salaam.

Judith Wambura alizaliwa mkoani Shinyanga tarehe 15 jun, 1979 kwa Martha na Lameck Isambua Mbibo ambao ndio wazazi wake. Inasemekana dada jide alianza kuimba akiwa na umri wa miaka saba, alianza kuimba kanisani kama ilivyo kwa wasanii wengi, bi shosti pia ni moja ya wasanii wa bongo flava wanaoishi kwenye ndoa kwa sasa.

Banana Zorro na Suzy Walele wakilishana keki siku ya harusi yao iliyofanyika katika ukumbi wa Msasani Beach Club jijini Dar - es- salaam. Banana pia ni masanii wa bongo flava ambaye amesha sepa kwenye kundi la ukapera.

Na kwa sasa nadhani huyu ndio atakaye fata tunamuombea kila la kheri mungu ampe wepesi katika hilo Amin inshaallah.

3 comments:

  1. Dulla sio msanii lakini pia unajulikana na wewe je tukusubiri lini kaka?

    ReplyDelete
  2. DAH... ME BADO NDUGU YANGU SI UNAJUWA KUOA NI KUJIPANGA LAZIMA UJIPANGE KWANZA LA SIVYO UTAWAPA WATU FAIDA...

    ReplyDelete
  3. From danix
    hope your turn will soon alive for you to live bachelor life.

    ReplyDelete

,