.

Thursday, December 3, 2009

JOH MAKINI AWA MAIND WANA WANAOPIGA MAGUMASHI KUPITIA MAUJANJA YAKE...

Mchizi kutoka Arusha Joh Makini amewalalamikia jamaa ambao wanatumia mashairi ya nyimbo zake kutengenezea tshirt , kwa mfano ngoma ya STIM ZIMELIPIWA tayari tshirt zimeshatoka nyingine ni MWAMBA WA KASKAZINI.

Makini anasema tshirt hizo hausiki nazo na anawaomba mashabiki zake kuto kuzinunuwa kwa sababu hazimuingizii chochote, na tayari anashughulikia ishu za kisheria kwa ajili ya hawa jamaa wanaopiga hayo magumashi.


Anasema mchizi mmoja anaitwa Luka wa Sinza kijiweni yeye ni moja kati ya hao wanaofanya hivyo, ameniambia nguo zake atazitowa muda si mrefu na zitapatikana kwenye duka la washkaji wa Maujanja Mwenge.

No comments:

Post a Comment

,