.

Tuesday, October 27, 2009

MISHE MISHE ZINAENDELEZWA KATIKA WANAWAKE LIVE SHOW.

Niliwa kukufahamisha kuhusu show inayoongozwa na mwanaharakati wa kike Bongo ambaye pia anafanya kipindi cha Bongo Movie kinachorushwa na EATV, show ambayo inahusu maswala ya wanawake wa kitanzania na pia anapata nafasi ya kuongea na wanawake ambao wapo katika sekta mbali mbali na waliofanikiwa kimaisha kwa ajili ya kuleta chachu ya mafanikio kwa wanawake wengine.
Hapa namzungumzia starring Joyce Kiria Nkongo, nilipata bahati ya kutembelea sehemu ambayo huwa ana record kipindi chake cha Wanawake Live Show na haya ndio yanayojiri huko....

Joyce Kiria Nkongo akifanya mahojiano na Mama Rahma huyu ni mwanamke mjasiliamali ambaye yeye shughuli zake ni kuchoma chapati na mafanikio yote ambayo yeye ameyapata katika maisha yake yametokana na hiyo kazi yake.

Kipindi hiki kinamuhusu kila mwanamke wa kitanzania hapa alikuwa akimuhoji Dinah Ismail (Mhariri gazeti la Tanzania Daima).

Hapa wakijitayarisha tayari kwa kuanza kurecord kipindi cha WANAWAKE LIVE SHOW.

Jamani yule sio keysher kweli mmmhh... embu ngoja nimvute zaidi......

Yeah... ndio mwenyewe kweli duh... kweli hii Wanawake Live Show haiyachi kitu huyu pia ni mwanamke ambaye amepata nafasi ya kuongea mawili matatu kuhusu Wanawake katika kipindi hiko... haya ngoja tuone kikishaanza kuruka hewani....

1 comment:

  1. ha, ha,ha kweli huu ndo mpango mzima, its from zero to hero! kip it hot joyce

    ReplyDelete

,