.

Friday, October 23, 2009

WANACHUO WATIMBA MZIGONI LEO.....

Hapa wanapokea maelezo kutoka kwa mkuu wa wa uzalishaji vipindi EATV Joshua Murunga jinsi vijana wake wanavyo piga mzigo.



Mkuu wa vipindi EATV akitoa maelezo kwa wageni.

Leo tulikuwa na ugeni wa kisomi kutoka chuoni sio choo...................ni nooooo...!! ni chuoni tuelewane hapo tafadhali naona imeshakuwa tabu sasa.... haya tuachane na hayo. Jamaa wanatokea ST. MARY'S TEACHERS COLLEGE hawa jamaa wanajifundisha uwalimu, kwakuwa bado hawajawa walimu sasa acha na sisi tuwafundishe kuhusu EATV kiujumla. Walikuja mzigoni kututembelea na kuangalia jinsi vipindi vinavyotengenezwa na mambo mengine tu kuhusu TV/RADIO, Walipata nafasi ya kujifunza mambo mbali mbali napia kutembelea studio za East Africa Radio pamoja na chumba chakurushia matangazo cha EATV , na mwisho wa sikuuuuu.... tukakamilisha lugha yetu kwambaaaaa.... 'TOGETHER TUNAWAKILISHA'Mimi napenda niwaite hiviii... Walimu wanafunzi.. wakiwa radio wakiangalia mzigo unavyo sukumwa.Kweli mwenye macho haambiwi tazama kila mtu yupo makini kuzungusha jicho lake.Umakini muhimu sehemu kama hizi ukizubaa utapitwa na mengi.EATV kwa kheriiiiii...... Baada ya kutembelea kila sehemu ilifika time ya wao kujisepesha kwa sababu darasa bado linawadai....

No comments:

Post a Comment

,