.

Thursday, November 5, 2009

FIESTA ONE LOVE LASOGEZWA MBELE

Tamasha la Fiesta One Love 2009 lililotarajiwa kufanyika jumamosi hii,Novemba 7 katika uwanja wa posta,kijitonyama jijini Dar,limeaihirishwa na kusogezwa mbele.


Akizungumza mratibu mkuu wa tamasha hilo Bw.Ruge Mutahaba amesema kuwa tamasha hilo limeaihirishwa hadi Novemba 21,mabadiliko hayo yanatokana na wahusika wakuu wakiwemo wafanyakazi wa Clouds Media Group/Prime Time Promotions (ambao kwa kiasi kikubwa ndiyo waandaji wa tamasha hilo) kuondokewa (kufariki) kwa Mwenyekiti wao Mzee Alex Mkama Kusaga juzi jioni nchini Afrika ya Kusini alikopelekwa kwa ajili ya matibabu.


Mutahaba amesema ratiba ya wasanii wambao walipaswa kushiriki kwenye tamasha hilo la Kitaifa iko pale pale wala haijabadilika,na kwamba msanii ambaye alitajwa angewatumbuiza wakazi wa Dar kutoka chini Marekani kwenye tamasha hilo,Buster Rhymes na wenzake naye ratiba yake iko pale pale,kwamba atakamua vilivyo siku hiyo. .
Aidha kwa taarifa za msiba wa Mzee K. inaelezwa kuwa mwili wake utawasili leo jioni na msiba upo nyumbani kwake Mbezi Beach karibu na Girrafe Hotel,kuhusu ratiba za mazishi na mambo mengine tutaendelea kufahamishana zaidi.

No comments:

Post a Comment

,