.

Wednesday, November 11, 2009

HII NDIO DIAMOND INAYO NG'ARA KWENYE BONGO FLAVA...!!!

Anaitwa Naseeb abdul Juma ni mmoja kati ya wasanii chipukizi ambao wametia maguu hivi karibuni katika dambwe hili la Bongo Flava mchizi ambaye kiukweli anaupenda sana muziki na ndio maana ana haha usiku kucha kutafuta mafanikio zaidi katika muziki huu.

Mwanzo alianza na ngoma ya Jisachi ambayo alimshirikisha Geez Mabovu pamoja na Mangwea ambapo mzigo alisimamiwa na Lamar kutoka Fish Crub, baada ya hapo mcharuko ukahamia kwenye ngoma nyingine ili kuwa inaitwa Wivu ambayo alimpa shavu ndugu yake Romen.

Baada ya mishe mishe zote hizo sasa dogo akaangukia penyewe ambapo raia walikuwa wanapataka, ameachia mkwaju mmoja matata sana unaitwa KAMWAMBIE kama bado hujausoma angalia Planet Bongo leo saa tatu usiku utaisoma..... Na kama kama ulikuwa humjuwi huyu ndio Diamond alidriki hadi kuiba pete ya dhahabu ya mama yake na kuuza kwa ajili ya kwenda kurecod duh...!!!!

No comments:

Post a Comment

,