.

Tuesday, November 24, 2009

HUYU NDIO K'NAAN...!!!!

Mchizi alizaliwa 1978 ni moja kati ya ma star wa kimataifa wanao ibuka na kupata mafanikio ya haraka sana katika mchakato mzima wa RAP - MUSIC.
Jamaa anatokea SOMALIA lakini alitoroka huko kitambo sana baada ya kukimbia vita vilivyo kuwa vikiendelea huko SOMALIA na kukimbilia TORONTO - CANADA.

K'naan albam yake ya kwanzan ilitoka mwaka 2000 "WHAT NEXT" albam hii ilimpatia mafanikio ingawa sio kivileeee...!!! na kwa sababu ilikuwa ndio mwanzo wake K'naan aliweza kuwa nominated mara tano katika tuzo za huko Toronto zinaitwa Toronto African Music Awards.

Kama unavyo juwa kombe la dunia, jumamosi ya tarehe 21 Nov lilitimba bongo.
Na K'naan ni mmoja kati ya watu wanao husika ipasavyo na kombe hilo kila liendapo kwa sababu mchizi yeye ndiye amepata fursa ya kuuandika wimbo Rasmi wa kombe la dunia mwaka huo 2010.

No comments:

Post a Comment

,